Jaji Mkuu wa Tanzania, Mhe. Prof. Ibrahimu Hamis Juma amewahakikishia Majaji Wateule kuwa uteuzi wao ni sahihi na hivyo wawe tayari kufanya kazi na Mahakama mara baada ya kuapishwa rasmi na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan.