Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan amewaapisha jumla ya Majaji wapya 28 huku akiwa na imani kuwa ongezeko hilo la Majaji saba (7) wa Mahakama ya Rufani na 21 wa Mahakama Kuu ya Tanzania litasaidia kupunguza tatizo la ucheleweshwaji wa kesi Mahakamani.